***SEHEMU YA A: FASIHI SIMULIZI***
***Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.***
*Malaika, nakupenda malaika*
*Malaika, nakupenda malaika*
*Nami nifanyaje?*
*Nashidwa na mali sina we*
*Nangekuoa malaika*
*Nashindwa na mali sina we*
*Ningekuoa malaika*
*Pesa, zasumbua roho yangu*
*Nashindwa na mali sina we*
*Ningekuoa malaika.*
***Maswali***
*(a) Tambua kipera cha wimbo huu. (alama 1)*
*(b) Thibitisha jibu lako la (a) (alama 2)*
*(c) Taja nafsi neni na nafasi nenewa wa wimbo huu. (alama 2)*
*(d) Fafanua mitindo **mitatu **iliyotumika katika wimbo (alama 3)*
*(e) Eleza umuhimu wa wimbo huu katika jamii. (alama 4)*
*(f) Ni vipi fanani anaweza kufanikisha uwasilishaji wa wimbo huu kwa hadhira yake? (alama 5)*
*(g) Unanuia kutumia njia ya kushiriki katika kufanya utafiti kuhusu wimbo huu. Eleza changamoto **nne **za kutumia njia hii. (alama 4)*